Chanzo kikuu cha nishati ya joto na umeme kitakacholisha viwanda vya kanda ya kusini na kuwasha taa za Tanzania nzima.
Mradi huu unatarajiwa kuzalisha takriban 600MW za umeme. Nusu ya umeme huu utatumika kwenye kiwanda cha chuma cha Liganga na nusu nyingine itaingizwa kwenye gridi ya taifa.
Makaa ya Mchuchuma yana sifa ya kipekee ya kuzalisha joto kali linalohitajika kuyeyusha chuma. Bila Mchuchuma, mradi wa Liganga hauwezi kufanya kazi kwa tija.
Ziada ya makaa ya mawe inaweza kuuzwa katika nchi jirani na masoko ya kimataifa, ikileta fedha za kigeni na kuimarisha uchumi wa Ludewa.
Mchuchuma na Liganga ni kama chanya na hasi. Liganga inatoa Chuma, Mchuchuma inatoa Nguvu. Kwa pamoja, wanatengeneza Mapinduzi ya Viwanda (Industrial Revolution) ya Tanzania.